KURASA

Sunday, January 3, 2010

MVUA NA MIUNDO MBINU YETU

Jamani heri ya mwaka mpya kwenu nyote, namshukuru MUNGU niko buheri wa afya, Leo nitawaonyesha baadhi ya picha zinazoonyesha tabu tunayopata tukiwa field kutokana na madhara ya mvua kwenye barabara ambazo si za lami, kwa kweli kuna sehemu hata gari ikiwa na 4wheel drive inaweza isipite, pia kunatakiwa uzoefu wa kuendesha kwenye barabara hizo, kama wewe ni dereva wa mjini kwenye lami tu basi kazi utakuwa nayo

TANGA







MANYARA


RUKWA





RUVUMA


Hivi mnategemea kwa kutumia barabara hizi mkulima ataweza kweli kusafirisha mazao yake na kuyapeleka mjini kwenye masoko au mazao hasa yale yanayooza haraka kama matunda na mboga mboga si yataharibikia shambani.