KURASA

Tuesday, May 5, 2009

LEUCAENA - VIBIRITI




Huu ni aina ya mti ambao unaweza kuukuta umeota mingi mingi pamoja kama kichaka au mmoja mmoja na kuwa mti mkubwa kabisa. Unastawi zaid sehemu za joto na kukua haraka, kwenye baridi ukuaji wake si wa haraka sana kama sehemu za joto, una mbegu nyingi sana zikiwa kwenye maganda mengi pia,
Upandaji wake ni kwa kukusanya mbegu zilizo komaa na kukauka na kisha kuzi mwaga sehemu unayotaka ziote kisha kuzifukia kwa udongo kiasi kidogo sana, upandaji ufanyike mara baada ya mvua za kwanza kuanza

MATUMIZI
(A)Mmea hu una protini nyingi sana kwenye majani yake kiasi cha asilimia 25%, kwa hiyo unafaa kwa ajili ya chakula cha mifugo kama ng’ombe, mbuzi, nguruwe na kuku. Unachanganya majani yake (makavu au mabichi) katika mlo wa wanyama. Kiasi cha lukina kisizidi asilimia 30% ya mlo kwa sababu kinaweza kusababisha wanyama kunyonyoka manyoya baada ya miezi 6 na pia kupata ugonjwa goita (goiter)



Kwa wafugaji wa nguruwe unaweza kutumia lukina 30% majani ya kawaida 70% na udongo mwekundu kama chanzo cha madini ya chuma kutengeneza mlo kamili kwa ajili ya nguruwe wako, inashauriwa pia kuwapa pig mix ili kuepukana na upungufu wa madini mengine.
Kwa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa changanya pumba 60% na lukina 40% na cattle mix kisha uwalishe kama chakula cha ziada chenye virutubisho(concentrates) wakati wa kukamua ng’ombe maziwa. Kwenye mlo kamili kumbuka lukina isizidi kiasi cha 30%
Pamoja na kuwa na madini mengine lakini mmea huu una kirutubisho kinachojulikana kama carotene ambacho husababisha wanyama wanaokula lukina kuwa na provitamin A nyingi sana kwenye nyama baada ya kuchinjwa. UVunaji wake ni kwakupunguza matawi na kama unahitaji kuhifadhi basi unakausha kwenye kivuli na majani yakipukutika unayakusanya na kuyatunza mahali pakavu.




(B) Lukina pia inaweza kutumika kwa ajili ya kuongeza kiasi cha nitrogen kwenye udongo kwa kupanda kati ya mimea au kwa wale wanaotumia kontua kwenye miteremko wakatumia kontua za lukina kwa kukinga mmong’onyoko wa udongo lakini isiache kukua na kuwa miti mikubwa labda kwa wale wanaohitaji kukinga upepo tu.



(C)Miti hii pia inaweza kutumika kwa ajili ya sehemu zilizokumbwa na balaa la kupoteza uoto juu ya ardhi, sababu kubwa ni ukuaji wake wa haraka na ikipandwa sehemu hata kama ni michache husambaa haraka kwa sababu inazalisha mbegu nyingi sana na zinasambaa kwa upepo ingawa haziendi mbali zaidi