KURASA

Friday, October 30, 2009

MABUA YA MAHINDI, NG'OMBE NA SAMADI-KUNA FAIDA HAPA

Unafahamu ni kiasi gani cha mabua kinabaki baada ya kuvuna shamba lako la mahindi? Jaribu kutazama vizuri shamba lako kwa macho na hutaamini !!!!!!!!!!! karbu nusu ya kile ulichovuna kimebaki shambani kama mabua yaani ile mbolea ya samadi uliyoweka bado iko shambani katika mfumo mwingine.

Mabua yanaweza kulishwa tena wakati wa ukame yakikatwa katwa na kuchamnganywa na molasses, ekari moja ya mabua intosha kumlisha ng’ombe mmoja mwenye kilo 500 kwa miezi miwili. Hili ni zoezi lenye lengo la kupunguza gharama na kuongeza faida lakini linahitaji umakini kidogo, ninashauri mara tu baada ya kumaliza kuvuna mabua haya nayo yavunwe na kuhifadhiwa sehemu yenye kivuli, na hao utaweza kumlisha mnyama wako mabua yakiwa na 65% chakula chakula mmeng’enyo (digestable food) huku kukiwa na protini kiasi cha 7%



Kama hunasehemu ya kuhifadhi mabua haya unaweza kuwachungia humo humo shambani ng’ombe wako ili wale wenyewe ila utahitajika kuwawekea mawe yenye madini ili walambe, kwa kuwachungia shambani ng’ombe wako utapata faida zifuatazo, kwanza hutahitaji kusafirisha mbolea ya samadi na kuirudisha shambani, pia nombe wanapo kanyaga shamba husaidia kupunguza mmong’onyoko wa udongo. Kama msimu uliopita ambao ndio mahindi yalilimwa kulikuwa na upungufu wa mvua inabidi uwe makini maana mabua yatakuwa na kiwango kikubwa cha madini ya nitrate ambayo yana madhara hasa kwa wanyama wanaokua wenye mimba au kunyonyesha, ili kuepuka hili unaweza kuwalisha wanyama wako chakula kingine kwanza na kumalizia na mabua au kama umeyakata basi changanya na majani mengine kasha ndio uwalishe. KUMBUKA ng’ombe mwenye kilo 500 anaweza kuzalisha molea hadi kilo 12 kwa siku je hii si faida kubwa?

Wednesday, October 14, 2009

TARATIBU NA MASHARTI YA MIKOPO YA KUNUNUA TREKTA JIPYA



1. Mwombaji atajaza fomu maalum ya maombi inayopatikana katika Ofisi za kilimo za Halmashauri za Wilaya na Makao makuu ya Mfuko wa Pembejeo, jijini Dar-es-salaam na katika tovuti ya wizara ya kilimo.

2. Fomu za maombi zilizojazwa na kuambatanishwa na vielelezo vinavyohitajika zitapitishwa/kuidhinishwa na Afisa Kilimo wa Maendeleo ya Mifugo wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya husika na baadaye kutumwa mapema kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Pembejeo.

3. Mikopo ya kununua matrekta inatolewa na Mfuko wa Pembejeo, baadhi ya benki na taasisi za fedha na SCCULT (T) Ltd. kwa niaba ya Mfuko, mwombaji sharti atimize yafuatayo:-

(A) Awe na dhamana yenye hati miliki isiyohamishika iliyoandikishwa kwa jina la mwombaji.
(B) Awe na shamba binafsi lisilopungua hekta 50 na awe tayari kutoa huduma ya kuwalimia wakulima wengine
(C)Awe tayari kutekeleza masharti yote ya Mfuko wa Pembejeo au taasisi ya fedha na SCCULT yanayohusu mkopo wa ununuzi wa trekta jipya.
(D)Awe tayari kulipa asilimia moja (1%) ya mkopo kama gharama za nyaraka za mkopo na kusajili trekta kwa pamoja kwa jina lake na Mfuko
(E) Riba inayotozwa ni asilimia nane (8%) na marejesho hufanyika kwa muda wa miaka mitatu kila baada ya miezi mitatu.

Saturday, October 10, 2009

KUKATA PEMBE NA KUZUIA PEMBE KUOTA

Mnyama asiye na pembe hasa ng’ombe hupunguza uwezekano wa wanyama kuumizana na hata kuwadhuru binadamu, wanyama wadogo kama miezi miwili hadi mitatu ni vizuri wakachomwa ili kuzuia pembe kuota (disbudding) lakini kama pembe zimetokeza hamna jinsi ila kuzikata kwa kutumia msumeno au waya maalum (phatetomy wire)

DISBUDDING IRONS


Zoezi la kuzuia pembe kuota hufanyika kwa kutumia vyuma maalum (disbudding iron) ambavyo hupashwa moto na kuwa vyekundu, ndama huandaliwa kwa kulazwa chini na kisha kupunguzwa manyoya sehemu itakayochomwa ambapo ni pale pembe zinakoota, unaweza kuitambua sehemu hii kwa kupapasa na utaona kama pembe ndogo ndani ya ngozi. Sehemu husika isafishwe kwa spirit au eusol kabla ya zoezi kuanza.



Mtaalamu wa mifugo ndiye atakaye fanya zoezi hili kwa kufuata kanuni za kitaalam, kabla ya kuanza zoezi ni muhimu mnyama kupigwa sindano ya ganzi, kisha sehemu husika huchomwa na chuma cha moto, na chuma kuzungushwa kila upande na mwisho kama anazibua ataondoa kile kipande kinachoota na kumalizia kwa kukausha sehemu iliyobaki kwa kutumia chuma kile kile, baada ya hapo dawa za kupulizia za vidonda, iodine tincture au dawa za kufukuza wadudu hupakwa sehemu husika na mnyama huachiwa huru.



Kuhusu ukataji wa pembe ambayo imeshaota, baada ya mnyama kufungwa na kulazwa chini huchomwa ganzi na ukataji huanza. Kama utatumia msumeno lazima damu nyingi itatoka, zuia damu hii kwa kuunguza sehemu ndogo ya pembe iliyobaki kwa kuichoma na disbudding iron au chuma chochote cha moto. Inashauriwa kutumia phatetomy wire kwa sababu wakati unakata pembe waya huu huunguza pembe na kufanya damu isitoke kabisa



Kuna baadhi ya aina za ngombe wa kisasa hazina pembe kabisa mfano Hereford na mbegu kama Friesian baadhi yao huwa hawana pembe, kwa mbegu za kienyeji kama zebu (SHZ)huwa na pembe fupi fupi

Saturday, October 3, 2009

KUKU WA KIENYEJI - UFUGAJI BORA




Kuku hutoka kwenye kizazi kinachojulikana kitaalam kama gallus gallus, Ufugaji huu nitaoelezea ni wa kienyeji kabisa ila huu umeboreshwa kidogo ili kuleta faida zaidi, kwanza itabidi uwe na eneo lakutosha kama ekari mbili (70m *140m) banda la kuku liwe linalohamishika na liwe limejengwa juu juu, hii husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa kwa sababu kinyesi cha kuku kikilundikana huweza kubeba vimelea vya magonjwa

BANDA BORA LINALOHAMISHIKA


Banda liwekewe viota vya kutagia na unaweza kuwafundisha kuku kuvitumia mapema kabla ya kuanza kutaga kwa kuchelewa kuwafungulia asubuhi. Kwa kawaida kuku hupenda kulala bandani wakiwa juu juu kwa hiyo uweke baadhi ya fito au mbao nyembamba zikining’inia pia kuwe na vyombo vya chakula nje ya banda

Hakikisha banda halivuji na wanyama wakali hawaingii lakini liwe na hewa ya kutosha na lisiwe na joto wala baridi kali, ni vizuri ukiliweka chini ya miti
Ili kuboresha ufugaji huu inashauriwa kutumia majogoo ya kisasa ambayo yana patika kwa mazalishaji wa kuku kote nchini, pia unaweza kutumia majogoo ya kuku aina ya KUCHI wanaopatikana zaidi miko ya Singida na Shinyanga. Majogoo ya kisasa huweza kuhudumia wastani wa majike 20-25 na kuchi huweza kuhudumia majike 10 -15 kwa sababu ni wavivu kidogo

MAJOGOO YA KISASA INA YA CORNISH


Andaa na banda la kukuziA watoto ambalo litawakinga na wanyama wakali na mwewe, banda linakuwa wazi juu hukulikizuiwa na waya kwa 75% na 25% iwe imezibwa kwa mbao ili kuwapatia kivuli wanapohitaji, banda hili lina hitaji kuhamishwa hamisha angalau mara 5 kwa siku kutika mahali pamoja hadi pengine, hakikisha banda la watoto lina maji na chakula muda wote, pia kumbuka kuwawekea mabaki ya mboga za majani kama mchicha, kunde, kisamvu n.k




FAIDA
(A) Mfumo hauhitaji chakula maalum kama kuku wa ndani
(B) Wadudu kama utitiri na virobot hushambulia kuku mara chache
(C) Kuku hupata muda wa mazoezi kwa kutembea tembea
(D) Gharama za uendeshaji ni kidogo
(E) Hautumii muda mwingi
(F) Kiasi cha uchafu ni kidogo

HASARA
(A)Vifaranga huweza kuliwa na mwewe au wanyama
(B) Mayai huweza kupotea yakitagwa nje ya banda
(C)Kuku huweza kula mbegu zilizopandwa mashambani
(D)Vifo vya kuku ni vingi

CHANJO
Kuku wapewe chanjo ya kideri/mdondo kila baada ya miezi mitatu chanjo hii hupatikana nchini kote ukifika dukani ulizia chanjo ya newcastle, utapata maelekezo ya jinsi ya kuwawekea kuku kwenye maji ya kunywa, chanjo hii wapewe kuku wazima tu na wagonjwa watengwe mbali

MINYOO
Kuku hunyweshwa dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu, kuna dawa kama piperazine na nyinginezo ambazo huwekwa kwenye maji

CHAWA NA UTITIRI
Unaweza kutumia dawa za kuogeshea mifugo kama ecotix au dawa ya unga unga ya kunyunyuzia kama akheri powder, dawa ya akheri unaweza kuimwaga bandani na kisha kumnyunyuzia kuku mwilini ukiwa umemning’iniza kichwa chini miguu juu ili mayoya yaacha nafasi ya dawa kuingia

MAGONJWA YA MAPAFU
Kuna magonjwa mengi yanayoshambulia mfumo wa hewa, dawa ya tylosin inauwezo mkubwa wa kupambana na magonjwa karibu yote, wape dawa hii mara tu unapoanza kuona dalili za mafua