KURASA

Monday, September 27, 2010

SIKU YA KICHAA CHA MBWA DUNIANI

Kila mwaka tarehe 28 ya mwezi wa tisa (september) ni siku ya kichaa cha mbwa duniani, hapa nchini serekali katika kampeni ya siku hii maalum imetoa kiasi cha chanjo 100,000 bure kwa mafugaji mbwa katika mikoa ta Dar es salaam, Mtwara, Lindi na Pemba

kutokana na takwimu za wizara ya mifugo na uvuvi inaonyesha mwaka jana watu 21,000 walingatwa na mbwa nchini Tanzania. Kati ya hao watu 51 walifariki dunia kwa sababu ya kichaa cha mbwa.

Ingawa kwa kiswahili ugonjwa huu unaitwa kichaa cha mbwa, lakini ukweli hushambulia hata wanyama wengine kama paka, ng'ombe, mbuzi, kondoo na hata binadamu, Ugonjwa huu kwa wanyama hauna dawa ila kinga tu kwanjia ya chanjo

Kuuelewa zaidi ugonjwa huu soma hapa
http://mitiki.blogspot.com/2009/08/kichaa-cha-mbwa.html

Thursday, September 23, 2010

DADA NAYMA ANAOMBA USHAURI ZAIDI

Hello Bro Bennet. Angalia miche yangu hatua iliyofikia bado sijaipeleka shambani,
naomba ushauri zaidi niliiotesha mwezi wa tano mwezi wa saba nikaiweka kwenye mifuko miche 300 tu.
nayma





Dada Nayma leo naomba nikuweke hadharani, wadau huyu dada nimekuwa nikimshauri kuanzia kuandaa mbegu, kitalu, kusia mbegu, umwagiliaji, kuhamisha mbegu kutoka kwenye kitalu hadi kwenye vipakti

Dada Nayma miche yako bado ni michanga kiasi, na kama unafuatilia utabiri wa mvua za msimu wa September mpaka November ni kwamba hakutakuwa na mvua za kutosha ila kwa mikoa ya kanda ya ziwa na zaidi Bukoba, nakushauri endelea kumwagilia miche yako ikue zaidi huku ukisubiri mvua za mwezi wa December mwishoni na January 2011, hapo itakuwa mikubwa ya kuweza kuhimili kama mvua zitakuwa chache

NB Hongera sana na anza kuandaa mbegu nyingine ili mwezi wa January uwe na miche mingi zaidi

KILA KAZI NA HATARI ZAKE

Leo nilikuwa nimekwenda kutibu mbwa 9 katika kampuni ya usafirishaji ijulikanayo kama Ruvuvu transport huko kurasini, mbwa hao walikuwa wanasumbuliwa na ugonjwa wa minyoo ya kwenye ngozi ujulikanao kama MANGE, ugonjwa huu husambazwa na viroboto wa mbwa


HAPA MBWA ANAANDALIWA



KUCHOMA SINDANO MBWA

Friday, September 17, 2010

SHARK - MKEMIA WA MAJI

Leo nilikuwa nabadili maji kwenye chombo cha kufugia samaki wa urembo (aquarium)baada ya kuweka maji masafi na kuwarudisha samaki wangu kuna kitu nikakigundua. Pamoja ya kwamba samaki wote ni wa urembo lakini kila mmoja anatabia yake, ni samaki wawili aina ya shark ambao wanauwezo wa kutambua maji kama yana kitu chochote kibaya, kwa mfano kama kemikali yoyote, chumvi au madini yoyote yale zaidi ya kiwango cha kawaida. Mara tu utakapowaweka kwenye maji ambayo hayako sawa basi utawaona wanakaa chini tu na wala hawaogelei kama kawaida yao.

Wakati narudishia mawe kwenye chombo chao yalisuguana na chenga chenga zake zikabadili ubora wa maji, ingawa hayakuwa na tatizo lolote kiafya lakini samaki hawa aina ya shark waliweza kugundua hilo na walikaa kama wanavyoonekana hapa kwenye picha mmoja aligeuka juu chini kama vile kafa.







Baada ya kuona wako hivo nikawasha pampu ya kuongeza hewa kwenye maji pamoja na filter baada ya dakika kama 10 samaki hao wakaanza kuogelea kama kawaida, angalia video hii


Hawa hapa kwenye video ni goldfish aina ya shubunkin, redcap na goldspike


Angel fish ni aina nyingine ya samaki nilionao


Huyu anajulikana kama catfish, nayeye kazi yake kubwa ni kisafisha vioo na urembo wa ndani, anauwezo pia wa kumla samaki yoyote aliyekufa bila ya wewe kuanza kuhangaika kumtoa