KURASA

Sunday, November 30, 2008

SAMAKI WA UREMBO (AQUARIUM FISH)

Baada ya kuongelea kilimo cha mitiki, sasa naomba nigeukie upande mwingine wa ufugaji wa samaki wa urembo majumbani au popote.

Samaki wa urembo wako aina nyingi, wanamahitaji na tabia tofauti, tumezoea kuona wengi wakifugwa kwenye vyombo vya kioo (aquarium) na mara chache kwenye mabwawa. Mara nyingi majumbani wanakuwa kwenye aquarium na kwa wale wazalishaji (breeders) wnazalisha na kukuza kwenye mabwawa, mara chache sana wanatumika kwa ajili ya urembo kwenye mabwawa


Samaki wako aina nyingi lakini kwa hapa Tanzania waliozoeleka sana ni goldfish, koi, angels, cichlids, barbs, sharks, parots, catfish, gupies, sotas, zebra na kadhalika, na mimi nitajaribu kuwachambua ufugaji na mazingira wanayohitaji kwa baadhi ya samaki ingawa mahitaji yao hayatofautiani sana