KURASA

Wednesday, February 18, 2009

MBILIMBI

MTI WA MBILIMBI (M-MBILIMBI)




Huu ni mmea unaopatikana sana sehemu za pwani kama Zanzibar, Tanga, Dar es salaam, Kibaha n.k Ni mmea ambao hauwezi kuhimili ukame wala baridi kali na unastawi zaidi kwenye mvua za kutosha na udongo usiotuamisha maji kabisa.


MATUMIZI


Miaka mingi mbilimbi zimekuwa zikijulikana kwa matumizi ya achali ndio maana sehemu nyingine mbilimbi zilitungwa jina la PICKLE FRUIT. Utengenezaji wa achali uko wa kuchanganya vitu tofauti tofauti kama nyanya, vitunguu, pilipili, ndimu, malimao, chumvi, maembe n.k ambavyo vinankuwa katika vipande vidogo vidigo, unaweka kwenye chupa na kuanika juani kwa siku kadhaa (ingawa baadhi huupika mchanganyiko huu)

Mbilimbi pia hutumika kutengenezea siki (vinegar) na mvinyo, hii mara nyingi hufanyika viwandani na sio majumbani kama ilivyo achali.

Mbilimbi pia ni dawa kwa magonjwa kama chunusi, kifua na kukohoa na mengineyo mengi. Ili kutibu kukohoa unatakiwa utafune mbilimbi kama tunda mara mbili mpaka tatu kwa siku ukichanganya na chumvi kupunguza ukali wake au unaweza kula mbilimbi zilizoiva ambazo ndio zina vitamin C zaidi ya mbichi. Majani na maua yake ni dawa ya vidonda, unaponda ponda na kufunga kwenye kidonda kwa siku kadhaa, pia yanapunguza uvimbe.

MAUA YA MBILIMBI



Mbilimbi mbichi ambazo ni kali huwa na acid ijulikanayo kama OXALIC kwa kiasi kingi hivyo huweza kutumika kungarishia vitu vilivyotengenezwa na chuma, shaba na aluminium kwa kusugulia na kisha kusafisha na maji safi