KURASA

Sunday, December 7, 2008

MAJANI NA MIMEA (aquatic plants)

Majani ni kitu muhimu sana katika ufugaji wa samaki, kazi ya majani ni kusafisha maji na kuweka mazingira ya uhasilia kwa samaki, kuna majani ya bandia lakinioiyanabakia kama urembo tu kwa sababu hayawezi kusafisha maji. Ili majani yakue kwa kiwango kizuri ni lazima mahitaji yafuatayo yazingatiwe


MWANGAZA
Mwanga wa kutosha unahitajika kwa ajili ya ukuaji wa majani na mimea ya majini, hii husaidia katika tengenezaji wa chakula kwa kutumia majani yake, mwanga wa tube lights ni mzuri zaidi ila usiwe mwingi sana kwa sababu utachangia ukuaji wa algae kwenye maji. kiwango cha mwanga kinachoshauriwa ni 1.5 watts kwa kila galon ya maji (1.5wpg), mfano tank la galon 20 linahitaji taa ya watts 30




MIZIZI
Mizizi ya mimea na majani inahitaji kujishikiza kwenye sakafu yenye udongo, changarawe au mchanga ili iweze kufyonza virutubisho, inashauriwa usiweke changarawe tu bali uchanganye na mchanga


VIRUTUBISHO
Ili mimea iweze kukua vizuri inahitaji virutubisho kama nitrogen, potasium, phosphorus, chuma na kadhalika, nitogen ambacho ni kirutubisho kikuu kinapatikana kwenye vinyesi vya samaki amabvyo vinatoka kama ammonia. Pia maji yenyewe na chakula cha samakikina madini haya kwa kiasi kidogo



CARBON-DIOXIDE
Hii ndio hewa inayotumiwa na mimea na inapatikana kutokana na samaki wanavyo pumua (respiration). Kwa kawaida samaki wanavuta oxygen na kutoa CO2 ambayo ndio inatumiwa na mimea, wingi wa upatikanaji wa hewa hii ya co2 inategemeana na wingi wa samaki.

1 comment:

Anonymous said...

Hongera sana kwa kutuelimisha juu ya ufugaji wa samaki,,,natumaini utaendelea kutuelimisha zaidi