KURASA

Friday, March 27, 2009

KOMA-MANGA



Huu ni mmea unaopatikana sana sehemu za pwani kama Zanzibar, DSm, Tanga, Mombasa,Mtwara na lindi, mmea huu huzaa matunda yake ambayo huanza na ua kama kawaida na kisha tunda lenyewe. Komamanga kama tunda huwa la kijani kwa nje iliyochanganyika na kahawia, na ukilipasua ndani utakutana na mbegu nyingi zenye rangi nyekundu ambayo hutofautiana kukolea rangi na ukubwa kutokana na aina mbalimbali (specie)



MATUMIZI
Tunda lenyewe linatumika kama dawa ya kuongeza nguvu za kiume kwa wanaume, na pia zinasaidia kukomaza mbegu za uzazi kwa wanawake na wanaume. jinsi ya kutumia ni kulikata kisha unatoa mbegu zake na kuzila kama chakula.




matumizi mengine ni kama dawa ya tumbo kuharisha, pia yanasaidia kupunguza sukari mwili kwa wale wagonjwa wa kisukari (kwa kiasi kidogo). maua yake yakipondwa na kuchanganywa namji yatoa dawa ya kuoshea vidonda na kupunguza uvimbe.

1 comment:

Subi Nukta said...

Ah, Bennet, hapa ndo nimefuraaahi nimefurahi! Yaani nimekumbukia enzi za utoto kwenda kutafuta komamanga na kuishia kupambana na nyuki na vile vijidudu vyeusi vinavyopenda kufuata harufu ya komamanga likeshapasuka!