KURASA

Friday, October 30, 2009

MABUA YA MAHINDI, NG'OMBE NA SAMADI-KUNA FAIDA HAPA

Unafahamu ni kiasi gani cha mabua kinabaki baada ya kuvuna shamba lako la mahindi? Jaribu kutazama vizuri shamba lako kwa macho na hutaamini !!!!!!!!!!! karbu nusu ya kile ulichovuna kimebaki shambani kama mabua yaani ile mbolea ya samadi uliyoweka bado iko shambani katika mfumo mwingine.

Mabua yanaweza kulishwa tena wakati wa ukame yakikatwa katwa na kuchamnganywa na molasses, ekari moja ya mabua intosha kumlisha ng’ombe mmoja mwenye kilo 500 kwa miezi miwili. Hili ni zoezi lenye lengo la kupunguza gharama na kuongeza faida lakini linahitaji umakini kidogo, ninashauri mara tu baada ya kumaliza kuvuna mabua haya nayo yavunwe na kuhifadhiwa sehemu yenye kivuli, na hao utaweza kumlisha mnyama wako mabua yakiwa na 65% chakula chakula mmeng’enyo (digestable food) huku kukiwa na protini kiasi cha 7%



Kama hunasehemu ya kuhifadhi mabua haya unaweza kuwachungia humo humo shambani ng’ombe wako ili wale wenyewe ila utahitajika kuwawekea mawe yenye madini ili walambe, kwa kuwachungia shambani ng’ombe wako utapata faida zifuatazo, kwanza hutahitaji kusafirisha mbolea ya samadi na kuirudisha shambani, pia nombe wanapo kanyaga shamba husaidia kupunguza mmong’onyoko wa udongo. Kama msimu uliopita ambao ndio mahindi yalilimwa kulikuwa na upungufu wa mvua inabidi uwe makini maana mabua yatakuwa na kiwango kikubwa cha madini ya nitrate ambayo yana madhara hasa kwa wanyama wanaokua wenye mimba au kunyonyesha, ili kuepuka hili unaweza kuwalisha wanyama wako chakula kingine kwanza na kumalizia na mabua au kama umeyakata basi changanya na majani mengine kasha ndio uwalishe. KUMBUKA ng’ombe mwenye kilo 500 anaweza kuzalisha molea hadi kilo 12 kwa siku je hii si faida kubwa?

4 comments:

John Mwaipopo said...

benett karibu tena maana ulipotea. au ulikuwa vijijini kufundisha kilimo.

Bennet said...

Mkubwa tunajiandaa na msimu mpya wa kilimo kwa hiyo muda mwingi nakuwa nje ya mji ambako hakuna network na hata nikirudi nakuwa nimechoka kiasi nakuwa mvivu kutumia internet

Unknown said...

Kakaaa!!
Hizi post ni za muda mrefu! Miye ni member mpya.. Ninahitaji sana ushauri na maoni katika ujasiriamali. Nimelima heka mbili za mipapai hapo Kimanzichana, nina kuku wa kienyeji kama 40 hivi, na hivi karibuni nimepata trekta aina ya Ford 7500.
Kwa uchanga wangu kwa fani nahitaji msaada wa mkopo wa jembe ne tela. Napatikana kwa 0787519910 ama moddyguyz@yahoo.com
Msaada kwenye tuta tafadhali....

Bryan Stefan Loan Firm said...

Habari Je, unahitaji mkopo wa haraka ili kutatua mahitaji yako ya kifedha? Tunatoa mikopo ya kuanzia 2,000.00 hadi 50,000,000.00, tunaaminika, tuna nguvu, tuna haraka na tunabadilika, hatuna hundi ya mkopo na tunatoa dhamana ya mkopo wa 100% ya kigeni wakati wa uhamisho. Pia tulitoa mkopo wowote wa sarafu yenye riba ya 2% kwa mikopo yote Ikiwa una nia, wasiliana nasi kupitia barua pepe hii: (bryanstefanloanfirm@gmail.com) (bryanstefanloanfirm@outlook.com) au WhatsApp: +919654763221