KURASA

Saturday, December 19, 2009

LEHEMU - CHOLESTEROL

Dada Mary Chuwa alipenda kujua kuhusu lehemu kwenye mafuta, kwa lugha ya kiingereza lehemu ni cholesterol, kwa kawaida kuna aina mbili za cholestrol low density lipoprotein na high density lipoprotein aina zote mbili zinatokana na balance ya kemikali mbili za mafuta zijulikanazo kama polyunsaturated fats na monounsaturated fats. kama hizi kemikali mbili zitabalance zitatengeneza low saturated fats ambazo ni high density lipoprotein, hii ni cholestrol nzuri kwa mwili wa binadamu kwa sababu haina madhara, ila kama polyunsaturated fats na monounsaturated fats hazita balance zitaengeneza low density lipoprotein ambayo ni cholestrol mbaya na inamadhara katika mwili wa binadamu.

Lehemu mbaya (low density lipoprotein) ikiingia mwilini huganda kwenye kuta za mishipa ya damu na kwenye moyo hivyo kufanya njia za damu kuwa nyembamba na kusababisha magonjwa ya moyo au kiharusi (stroke)

Mafuta yatokanayo na Alizeti, karanga na mahindi kwa asili huwa hayana lehemu mbaya an hivyo kuwa salama kwa matumizi ya binadamu. Mafuta ya mawese, nazi, na yale yatokanayo na wanyama pamoja na mazao ya maziwa huwa na lehemu mbaya

Mikoa ya Singida na Manyara imekuwa ikizalisha kwa wingi sana alizeti na kuna viwanda vya kukamua mafuta sehemu hizo, kwa hiyo nashauri kama unaweza agizia mafuta halisi ya alizeti toka sehemu hizo, mbegu za alizeti hukamuliwa ilikupata mafuta na baada ya hapo mafuta huchemshwa na kuchujwa kisha kuwekwa kwenye madumu tayari kwa kuuzwa.

Ili kupunguza lehemu mwilini mwako inashauriwa kutumia asali kijiko kimoja na mdalasini nusu kijiko kila asubuhi kabla hujala chochote, unaweza kutia kwenye chai au maji ya moto mchanganyiko huu.
nakaribisha maoni kwa wenye ufahamu zaidi

2 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Kaka Beneth
Kwa niaba ya familia yangu na wapenda mema wote nakutakia kila lililo jema wakati huu wa sikukuu na usalama kuelekea mwaka mpya
Baraka kwako

Anonymous said...

Mchango wako una manufaa sana! Maparachichi na walnuts pia hupunguza bad cholesteral mwilini.Kupunguza kula nyama ya ng'ombe, mbuzi, kiti moto pia inasaidia, kupunguza idadi ya mayai mtu anayokula kwa wiki. Mbali na kuongelea upande wa ulaji, kufanya mazoezi pia kunasaidia kupunguza cholesteral mwilini na kula vyakula vyenye roughage nyingi, watu wnapaswa waelewe kuwa kipato kikiongezeka wasiache kufanya mazoezi na kutegemea sana technologia.