KURASA

Wednesday, December 30, 2009

MNYAUKO FUSARI - COFFEE FUSARIUM

Ugonjwa huu husababishwa na vimelea vya fusari. Hushambulia mashina, machipukizi na hata punje. Ugonjwa wa mnyauko fusari unashamiri kwenye mashamba ambayo hayatunzwi vizuri inavyopasa. Viini vya ugonjwa huu vinauwezo mdogo sana wa kushambulia
mkahawa wenye afya nzuri, ukiona shamba limeshambuliwa na uonjwa huu jua moja kwa moja kwamba shamba hilo halitunzwi vizuri kwa kufuata kanuni za kilimo bora.

DALILI KUU:

Machipukizi yaliyoshambuliwa na ugonjwa huu hunyauka, na majani hubadilika na kuwa na rangi ya kahawia. Matawi na mashina yakishambuliwa hunyauka na kufa. Ukitaka kuthibitisha dalili za fusari kata shina utaona miviringo ya kahawia. (Brown ring)

JINSI YA KUZUIA
• Palizi ni muhimu kwenye shamba.
• Ukataji sahihi wa matawi.
• Matumizi ya mbolea kwa kiwango kinachoshauriwa.
• Ng’oa na choma moto mikahawa iliyokufa.
• Iwapo ni matawi yanayoonyesha dalili za ugonjwa matawi hayo yakatwe na kuchomwa moto.

NB: Miche mingine ya kahawa isipandikizwe sehemu ilikong’olewa
mikahawa yenye ugonjwa kabla ya miezi sita.

SALAMU ZA MWAKA MPYA

Jamani kwa mwaka huu hii ni makala yangu ya mwisho, mwenyezi Mungu akinijaalia nitaendelea mwakani kuwaletea makala nyingine, mwaka huu Mungu aliniwezesha kutuma jumla ya makala 77 ambazo naamini kuna watu zimewasaidia na kuwanufaisha, kuna wengine wamekuwa wakiniuliza maswali kwa faragha na hawakupenda nichapishe majina yao nawashukuru sana, kuna wale walioanzisha mashamba mapya au walikuwa na mashamba na walihitaji ushauri wa kitaalam nao nilishirikiana nao vizuri, kuna ambao walitaka msaada wangu walipata lakini walishindwa gharama za mradi nawaombea kwa Mungu awawezeshe kupata pesa za kuanzisha miradi hiyo, Kuna nilio wakwanza kwa kushindwa kuwasaidia, inawezekena nilibanwa na ratiba au ushauri wangu haukuwa na manufaa kwao na wale walioshindwa gharama za ushauri (ingawa ni sawa na bure) NAOMBA WANISAMEHE

6 comments:

chib said...

Nakutakia heri ya mwaka mpya Bennett

Bennet said...

Asante KAka

Anonymous said...

Mbona uko shamba na hujavaa gum boot, wewe ndio unatakiwa kuwa mfano wa kuigwa hapo umeniangusha wangu

Bennet said...

Anony 11:54 jan 5
Miguu yangu huwa inatoka jasho sana, nikivaa gum boot miguu inateleza ndani kwa ndani na vidole vinaumia vikifika mbele, siku zote utaniona navaa hivi labda kama ni kwenye majaluba ya mpunga

Unknown said...

KAMA NATAKA USHAURI WA KILIMO CHA MAHINDI NA ALIZETI NIUPATA KWA BEI GANI?

NAOMBA GHARAMA ZA KILIMO CHA MAHINDI NA ALIZETI KWA HEKTA MOJA

FROM SALIM

Anonymous said...

YOU ARE GOOD MAN, KEEP IT UP,MIMI NIPO USA NITAKUTAFUTA VERY SOON MAANA NITAKUWA NATAFUTA KASEHEMU KA KULIMA MBOGA,benedictm12@yahoo.com. THANKS