KURASA

Sunday, February 7, 2010

MBUZI WA MOROCCO

Mbuzi unaowaona pichani hupatikana nchini MOROCCO, inasemekana ni kawaida kuwaona mbuzi wakiwa wamepanda juu ya hivyo vichaka ni kwa sababu wanafuata matunda yajulikanayo kama ARGO, kutokana na kuyapenda sana matunda hayo basi mbuzi hao hudandia juu ya matawi ya vichaka ili kupata matunda hayo



5 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Duh! mbuzi wa ajabu kweli hao sijawahi kuona hii. Jumapili njema kaka Bennet

Bennet said...

Nashukuru Dada Yasinta, sasa hivi nimebanwa kidogo ndio maana sipatikani sana kwenye mtandao

chib said...

Nakwambia... shida inafundisha mambo mengi.
Si ajabu tukasikia kuna sehemu kuku wanapiga mbizi kukamata samaki pale uhaba wa majani utakapotokea sehem sehemu :-)

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Pengine Charles Darwin alikuwa sahihi. Si ajabu baada ya miaka milioni moja ukakuta mbuzi hawa wamebadilika kwa kuota makucha, kuwa wembamba n.k. Mazingira na shida zinatufanya tuwe tulivyo!

John Mwaipopo said...

hivi nyama ya mbuzi inakiwango gani cha usababishi wa gout? how safe is nyama ya nguruwe?