KURASA

Saturday, October 9, 2010

KITUO CHA KUFUGIA SAMAKI MOROGORO MJINI BOMA ROAD

Nilibahatika kutembelea vituo vya ufugaji na uzalishaji wa samaki huko Morogoro mjini barabara ya boma na Kingolwira, mwenyeji wangu alikuwa ni Bwana Melton Kalinga ambapo tulishinda karibia kutwa nzima akinionyesha vitu mbali mbali huku tukibadilishana uzoefu na utaalamu wa kuzalisha samaki, wakati yeye alikuwa akinifundisha namna ya kuzalisha Sato na Kambale, mimi nilimfundisha namna ya kuzalisha samaki wa mapambo hasa Gold fish na Angels

HAPA NI MOROGORO MJINI BOMA ROAD kwenye kituo cha kufugia samaki, kuna mabwawa ambapo samki hufugwa baada ya kuzalishwa katika kituo cha Kingolwira


CHANZO CHA MAJI ni kutoka katika kisima cha kuchimbwa na maji huvutwa kwa pampu ya umeme





BANDA LA BATA kinyesi chao chakula cha samaki, pia wakiogelea husaidia kuingiza hewa kwenye bwawa (aeration)


SEHEMU YA KUWEKEA CHAKULA CHA SAMAKI sehemu hii imejengwa kwa kutumia miti na inahamishika


SEHEMU YA KUWEKEA CHAKULA CHA SAMAKI imejengwa kwa saruji, ni sehemu ya kudumu


BATA pia hufukuza ndege wanaokula samaki na kuwala vyura wala samaki


NDEGE MLA SAMAKI naye alikuwepo

3 comments:

Unknown said...

Mambovipi kaka shidayangu kubwa ni kuweza kuwazalisha goldfish tafadhali naomba msaadawako

Unknown said...

Mambovipi kaka shidayangu kubwa ni kuweza kuwazalisha goldfish tafadhali naomba msaadawako

Unknown said...

Je inamchukua mda gani mfugaji kubadili maji katika bwawa la kufugia samaki?