KURASA

Wednesday, July 25, 2012

TARATIBU NA MASHARTI YA MKOPO WA KUKARABATI TREKTA



1. Mwombaji atajaza fomu maalum ya maombi inayopatiakana kwenye ofisi za Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa na kweye tovuti ya mfuko. Fomu hii itapitishwa na Afisa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya husika.

2.  Afisa Zana katika Halmashauri watashirikiana na mmiliki pamoja na fundi wake kufanya tathmini ya kiwango cha ubovu wa matrekta hayo katika maeneo yaliyoanishwa katika taarifa ya tafiti za awali ya ukarabati. Mapendekezo yazingatie kiwango cha matengenezo ili gharama za vipuri na fundi zisizidi kiwango cha juu kinachoweza kutolewa.

3. Mwombaji atachagua Mtengenezaji/Fundi kutoka  kwenye  orodha ya  kampuni zitakazoingia mkataba na Mfuko wa Pembejeo. Mtengenezaji/Fundi atafanya ukarabati chini ya usimamizi na ukaguzi wa Afisa Zana. Mtengenezaji/Fundi atawajibika kutoa hati ya kuthibitisha ubora wa kazi/matengenezo na gerentii  ya  miezi  sita  kwa  vipuri vilivyokarabatiwa.

4.  Fomu za maombi pamoja na vielelezo vinavyohitajika zitatumwa kwa Mkurugenzi Mtendaji, Mfuko wa pembejeo.

5.  Dhamana ya mkopo huu ni kadi halisi ya trekta na mali nyingine isiyohamishika.

6. Muda wa mkopo ni mwaka mmoja na nusu kwa riba ya asilimia nane (8%).

7.  Mwombaji sharti awe tayari kutoa huduma ye kukodisha trekta hilo kwa wakulima wenzake

No comments: