KURASA

Tuesday, February 7, 2017

CHANJO ZA KUKU - RATIBA MAALUM

1.     SIKU 1. 
 Baada ya vifaranga kutotoleshwa ndani ya siku moja wapewe glucose kwa muda wa masaa mawili. Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa na baada ya hapo vifaranga wapewe mchanganyiko wa vitamins mfano ni AMINOVIT na OTC plus


Pia hii huchanganywa na maji. Vifaranga wawekwe katika eneo lenye joto wastani na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifaranga wapewe


2.       SIKU YA 7. 
vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDERI). chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kIsha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye mchanganyiko wa vitamini 


3.     SIKU YA 14. 
Wapewe chanjo ya GUMBORO(IBD). Chanjo hii pia huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili tu, baada ya hapo vifaranga wepewe mchanganyiko wa vitamin. Kuku waliokufa kwa ugonjwa huu unaweza kuwatambua kwa kuchana vifua vyao na hapo utaona vidoti vyekundu kama hapo pichani


4.     Siku ya 21 (wiki ya tatu) 
Rudia chanjo ya Newcastle (Kideri) 


5.     SIKU 28 (Mwezi) 
Rudia chanjo ya GUMBORO IBD 


6.     SIKU 35 (Mwezi 1 na wiki 1) 
Kipindi hiki kuku wapewe mchanganyiko wa vitamin ya kutosha. 


7.     WIKI YA 6-8 
KUKU wapatiwe kinga ya Ndui (fowl pox).kinga hii sio rahisi kwa mfugaji asiye na utaalam kuwapa kuku, tafuta mtaalum wa mifugo kwa kazi hii au upate maeleze ya jinsi ya kuweka kinga hii.


8.    WIKI YA 8 

Kuku wapatiwe dawa ya minyoo kama Piperazzine na baada ya hapo unaweza kurudia chanjo ya Newcastle

3 comments:

Unknown said...

Ahsante kwa makala hii nzuri, ila hujafafanua huo utaratibu wa chanjo uliouainisha hapo juu kama ni maalum kwa kuku wa aina gani: kienyeji, chotara au kisasa?

moseally said...

swali zurii

Ally Mkwanda said...

thanks for your good articles