KURASA

Friday, April 23, 2010

FUNGATE LA MKULIMA

Tukiwa na babu na bibi yangu mzee Msumari nyumbani kwake Makorora Tanga, huyu ni mdogo wa mwisho wa Bibi mzaa Baba na ndiye aliyebakia pekee



Tunapata msosi na my wife wangu tukiwa kijijini kwetu, hapa ni Ugali, kuku wa kienyeji na Mchunga bila kusahau ngogwe na chachandu la mbilimbi halafu tunashushia na mnazi au boha



Kaburi la Marehemu Baba yangu mzee Reginald Bennet huko Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga




Hili ni kaburi la marehemu Bibi mzaa Baba aitwaye Perpetua Mohamed kijijini kwetu Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga


Wife akishangaa machungwa, yakiwa madogo hivi tunaita mawashata taa



NB Picha za tukiwa Lushoto na Pangani sitaziweka humu kutokana na maombi ya mke wangu (privacy)

5 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Kwa kweli inapendeza sana kuwa nyumbani imenikumbusha mbali sana Ahsante kaka Bennet, wifi na familia yote kwa taswira hii nzuri. Muwe na wakati mzuri.UPENDO DAIMA.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Unapoamka NGOGWE jamani mate yamejaa kwa MUDOMO.

Yes, kuwa home ni bomba sana kwani nadhani umeona shamba ili uendeleze kazi katika spirit ya KILIMO KWANZA

Anonymous said...

Taswira nzuri saana, inapendeza kukumbuka asili yetu,,,taswira nzuri saana,,nakutakia maisha mema na yenye baraka tele ,,,,,Mungu awatangulie katika kila jambo

Baraka Mfunguo said...

Hongereni sana

Anonymous said...

Hongera sana kaka, nakutakia kila la kheri. Nimefurahi sana kukuona na kuona jinsi gani unaisaidia jamii. Be blessed.