KURASA

Saturday, September 17, 2011

MBEGU BORA YA MIHOGO YAGUNDULIWA

SHAMBA DARASA LA MIHOGO




Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ikishirikiana na taasisi ya kimataifa ya kilimo cha kitropiki (IITA) kwa pamoja zimezalisha aina mpya ya mbegu za mihogo zenye kustahimili magonjwa makubwa ya zao hilo. Mbegu hiyo mpya inayojulikana kama KIROBA inatoa wanga mzuri kwa ajili ya lishe na kuhimili magonjwa, pia inaweza kutoa mazao kufikia tani 35 kwa hecta.


MIHOGO BORA TAYARI KUVUNWA



Akiongea hayo Meneja wa mradi wa Shirika la chakula Duniani (FAO) BW. Raphael Laizer wakati anakagua mashamba darasa ya mihogo huko Mkuranga, alisistiza kutumia mashamba darasa ya zao la muhogo kwa ajili ya majaribio ili kupata mbegu bora ambazo zitalimwa karibu mikoa yote na ziwe zenye uwezo wa kuhumili ukame na magonjwa pia.

MIHOGO YA KUKAUSHA (makopa) KWA AJILI YA UNGA

4 comments:

Anonymous said...

Nashukuru sana kaka kwa taarifa nzuri ya mbegu mpaya ya muhogo. Nashukuru pia kuwa umekumbuka kuendelea kutuletea uhondo wa maarifa mengi ya kilimo. Mimi huwa kila siku natembelea hapa ingawa ni muda mrefu hujatuma post hapa. Nimeandika kukutia moyo kuwa usikae kimya muda mrefu hivyo.

ShooGAP

Anonymous said...

Hello Ben,
Pole na majukumu.
Naweza pata wapi hii mbegu mpya ya muhogo (kiroba)?? Inachukua muda gani mpaka zao kukomaa kwa mbegu hii mpya?? Nakushukuru sana kwa darasa lako.

Mdau

Ngassa Man said...

Nakupongeza kwa kuutumia vyema muda wako kukusanya habari njema kwa wakulima wa Tz

RULE STYLE said...

http://www.mebgu.ru/